Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 1:25-31 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Nitanyosha mkono wangu dhidi yenu;nitayeyusha uchafu wenu kabisa,na kuondoa takataka yenu yote.

26. Nitawapeni waamuzi wenu kama kwanzana washauri wenu kama pale awali.Ndipo Yerusalemu utakapoitwa ‘Mji wa Uadilifu’utaitwa ‘Mji Mwaminifu’”

27. Mji Siyoni utakombolewa kwa haki,uadilifu utawaokoa watakaotubu humo.

28. Lakini waasi na wenye dhambiwote wataangamizwa pamoja;wanaomwacha Mwenyezi-Mungu watateketezwa.

29. Mtaionea aibu hiyo mialoni mliyoipenda sana;mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizofurahia.

30. Mtakuwa kama mwaloni unaonyauka majani;kama shamba lisilo na maji.

31. Wenye nguvu watakuwa kama majani makavu,matendo yao yatakuwa kama cheche za moto.Watateketea pamoja na matendo yao,wala hapatakuwa na mtu wa kuwaokoa.

Kusoma sura kamili Isaya 1