Agano la Kale

Agano Jipya

Isaya 1:22-30 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Fedha yenu imekuwa takataka;divai yenu imechanganyika na maji.

23. Viongozi wako ni waasi;wanashirikiana na wezi.Kila mmoja anapenda hongo,na kukimbilia zawadi.Hawawatetei yatima,haki za wajane si kitu kwao.

24. Kwa hiyo asema Bwana Mwenyezi-Mungu,Mwenye Nguvu wa Israeli:“Nitawamwagia maadui zangu hasira yangu,nitawalipiza kisasi wapinzani wangu.

25. Nitanyosha mkono wangu dhidi yenu;nitayeyusha uchafu wenu kabisa,na kuondoa takataka yenu yote.

26. Nitawapeni waamuzi wenu kama kwanzana washauri wenu kama pale awali.Ndipo Yerusalemu utakapoitwa ‘Mji wa Uadilifu’utaitwa ‘Mji Mwaminifu’”

27. Mji Siyoni utakombolewa kwa haki,uadilifu utawaokoa watakaotubu humo.

28. Lakini waasi na wenye dhambiwote wataangamizwa pamoja;wanaomwacha Mwenyezi-Mungu watateketezwa.

29. Mtaionea aibu hiyo mialoni mliyoipenda sana;mtafadhaika kwa sababu ya bustani mlizofurahia.

30. Mtakuwa kama mwaloni unaonyauka majani;kama shamba lisilo na maji.

Kusoma sura kamili Isaya 1