1. Msifurahi enyi Waisraeli!Msifanye sherehe kama mataifa mengine;maana, mmekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu.Mmefurahia malipo ya uzinzi,kila mahali pa kupuria nafaka.
2. Lakini ngano na mapipa ya divai haitawalisha,hamtapata divai mpya.
3. Hawatakaa katika nchi ya Mwenyezi-Mungu;naam, watu wa Efraimu watarudi utumwani Misri;watakula vyakula najisi huko Ashuru.
4. Hawatamtolea Mwenyezi-Mungu sadaka ya divai,wala hawatamfurahisha kwa tambiko zao.Chakula chao kitakuwa kama cha matanga,wote watakaokila watatiwa unajisi.Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu,hakitafaa kuletwa nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.
5. Mtafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa,au katika karamu ya Mwenyezi-Mungu?
6. Mtakapoyakimbia maangamizi ya nchi yenu,Misri itawakaribisheni kwake,lakini makaburi yenu yawangoja huko Memfisi.Magugu yatamiliki hazina zenu za fedha,miiba itajaa katika mahema yenu.