Agano la Kale

Agano Jipya

Hosea 9:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Msifurahi enyi Waisraeli!Msifanye sherehe kama mataifa mengine;maana, mmekuwa wazinzi kwa kumwacha Mungu wenu.Mmefurahia malipo ya uzinzi,kila mahali pa kupuria nafaka.

2. Lakini ngano na mapipa ya divai haitawalisha,hamtapata divai mpya.

3. Hawatakaa katika nchi ya Mwenyezi-Mungu;naam, watu wa Efraimu watarudi utumwani Misri;watakula vyakula najisi huko Ashuru.

4. Hawatamtolea Mwenyezi-Mungu sadaka ya divai,wala hawatamfurahisha kwa tambiko zao.Chakula chao kitakuwa kama cha matanga,wote watakaokila watatiwa unajisi.Kitakuwa chakula cha kuwashibisha tu,hakitafaa kuletwa nyumbani kwa Mwenyezi-Mungu.

5. Mtafanya nini katika sikukuu ile iliyopangwa,au katika karamu ya Mwenyezi-Mungu?

6. Mtakapoyakimbia maangamizi ya nchi yenu,Misri itawakaribisheni kwake,lakini makaburi yenu yawangoja huko Memfisi.Magugu yatamiliki hazina zenu za fedha,miiba itajaa katika mahema yenu.

Kusoma sura kamili Hosea 9