Agano la Kale

Agano Jipya

Hosea 5:1-9 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Haya! Sikilizeni enyi makuhani!Tegeni sikio, enyi Waisraeli!Sikilizeni enyi ukoo wa kifalme!Nyinyi mlipaswa kuzingatia haki,badala yake mmekuwa mtego huko Mizpa,mmekuwa wavu wa kuwanasa huko Tabori.

2. Mmechimba shimo refu la kuwanasa huko Shitimu.Lakini mimi nitawaadhibuni nyote.

3. Nawajua watu wa Efraimu,Waisraeli hawakufichika kwangu.Nyinyi watu wa Efraimu mmefanya uzinzi,watu wote wa Israeli wamejitia najisi.

4. “Matendo yao yanawazuia wasimrudie Mungu wao.Mioyoni mwao wamejaa uzinzi;hawanijui mimi Mwenyezi-Mungu.

5. Kiburi cha Waisraeli chaonekana wazi;watu wa Efraimu watajikwaa katika hatia yao,nao watu wa Yuda watajikwaa pamoja nao.

6. Watakwenda na makundi yao ya kondoo na ng'ombe,kumtafuta Mwenyezi-Mungu;lakini hawataweza kumpata,kwa sababu amejitenga nao.

7. Wamevunja uaminifu kwa Mwenyezi-Mungu,wamezaa watoto walio haramu.Mwezi mwandamo utawaangamiza,pamoja na mashamba yao.

8. “Pigeni baragumu huko Gibea,na tarumbeta huko Rama.Pigeni king'ora huko Beth-aveni.Enyi watu wa Benyamini, adui yenu yuko nyuma!

9. Siku nitakapotoa adhabuEfraimu itakuwa kama jangwa!Ninachotangaza miongoni mwa makabila ya Israeli,ni jambo litakalotukia kwa hakika.

Kusoma sura kamili Hosea 5