1. “Haya! Sikilizeni enyi makuhani!Tegeni sikio, enyi Waisraeli!Sikilizeni enyi ukoo wa kifalme!Nyinyi mlipaswa kuzingatia haki,badala yake mmekuwa mtego huko Mizpa,mmekuwa wavu wa kuwanasa huko Tabori.
2. Mmechimba shimo refu la kuwanasa huko Shitimu.Lakini mimi nitawaadhibuni nyote.
3. Nawajua watu wa Efraimu,Waisraeli hawakufichika kwangu.Nyinyi watu wa Efraimu mmefanya uzinzi,watu wote wa Israeli wamejitia najisi.
4. “Matendo yao yanawazuia wasimrudie Mungu wao.Mioyoni mwao wamejaa uzinzi;hawanijui mimi Mwenyezi-Mungu.