Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 8:6-13 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Watenge Walawi kutoka Waisraeli, uwatakase.

7. Hivi ndivyo utakavyowatakasa: Wanyunyizie maji ya kutakasia kisha uwaambie wajinyoe mwili mzima, wafue nguo zao na kujitakasa.

8. Kisha watatwaa fahali mmoja mchanga pamoja na sadaka yake ya nafaka, yaani unga laini uliochanganywa na mafuta; nawe utatwaa fahali mwingine mchanga kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi.

9. Kisha utawakusanya watu wote wa Israeli na kuwaleta Walawi mbele ya hema la mkutano.

10. Utakapowaleta Walawi mbele yangu, Waisraeli watawawekea Walawi mikono,

11. halafu Aroni atawaweka hao mbele yangu kama sadaka ya kutikiswa kutoka kwa Waisraeli wanihudumie.

12. Kisha Walawi wataweka mikono yao juu ya vichwa vya fahali hao; mmoja wao utamtoa kuwa sadaka ya kuondoa dhambi, na huyo mwingine utamtoa kuwa sadaka ya kuteketezwa inayotolewa kwangu, ili kuwafanyia upatanisho Walawi.

13. “Kisha utawasimamisha Walawi mbele ya Aroni na wanawe na kuwaweka mbele yangu kama sadaka ya kutikiswa.

Kusoma sura kamili Hesabu 8