Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 7:56-71 Biblia Habari Njema (BHN)

56. kisahani kimoja cha dhahabu cha gramu 110 kilichokuwa kimejazwa ubani;

57. fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;

58. beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi;

59. mafahali wawili, kondoo madume watano, beberu watano na wanakondoo madume watano wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka za amani. Hiyo ndiyo iliyokuwa sadaka ya Gamalieli mwana wa Padasuri.

60. Siku ya tisa ikawa zamu ya Abidani mwana wa Gideoni, kiongozi wa kabila la Benyamini.

61. Sadaka yake ilikuwa: Sahani moja ya fedha ya kilo moja u nusu na bakuli moja la fedha la gramu 800, kulingana na vipimo vya hema takatifu, sahani na bakuli vilikuwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka;

62. kisahani kimoja cha dhahabu cha gramu 110 kilichokuwa kimejazwa ubani;

63. fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;

64. beberu mmoja kwa ajili ya sadaka kuondoa dhambi;

65. fahali wawili, kondoo madume watano, beberu watano na wanakondoo madume watano wa mwaka mmoja kwa ajili ya tambiko ya sadaka ya amani. Hiyo ndiyo iliyokuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gideoni.

66. Siku ya kumi ikawa zamu ya Ahiezeri mwana wa Amishadai, kiongozi wa kabila la Dani.

67. Sadaka yake ilikuwa: Sahani moja ya fedha ya kilo moja u nusu na bakuli moja la fedha la gramu 800, kadiri ya vipimo vya hema takatifu; sahani na bakuli vilikuwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kwa ajili ya sadaka ya nafaka;

68. kisahani kimoja cha dhahabu cha gramu 110 kilichokuwa kimejazwa ubani;

69. fahali mmoja wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;

70. beberu mmoja kwa ajili ya sadaka ya kuondoa dhambi;

71. fahali wawili, kondoo madume watano, beberu watano na wanakondoo madume watano wa mwaka mmoja kwa ajili ya sadaka ya amani. Hiyo ndiyo iliyokuwa sadaka ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.

Kusoma sura kamili Hesabu 7