Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 6:6-10 Biblia Habari Njema (BHN)

6. Siku zote atakazokuwa amejiweka wakfu kwa Mwenyezi-Mungu, mtu huyo asikaribie maiti,

7. hata kama ni ya baba, mama, ndugu au dada yake, asije akajitia unajisi kwa maana amejiweka wakfu kwa Mwenyezi-Mungu kwa kiapo.

8. Muda wote atakaokuwa mnadhiri atakuwa wakfu kwa Mwenyezi-Mungu.

9. “Endapo nywele za mnadhiri zitatiwa unajisi mtu afapo ghafla karibu naye, atakinyoa kichwa chake wakati wa siku ya kutakaswa kwake; atakinyoa katika siku ya saba.

10. Katika siku ya nane atapeleka hua wawili au makinda mawili ya njiwa kwa kuhani penye lango la hema la mkutano.

Kusoma sura kamili Hesabu 6