21. “Hiyo ndizo sheria inayomhusu mnadhiri anayeahidi kwa kiapo. Sadaka yake kwa Mwenyezi-Mungu ilingane na nadhiri yake, licha ya chochote kingine anachoweza kutoa; atafanya kulingana na nadhiri aliyoweka, kadiri ya sheria ya kujiweka wakfu kwake.”
22. Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose,
23. “Mwambie Aroni na wanawe kwamba hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli: Mtawaambia,
24. ‘Mwenyezi-Mungu awabariki na kuwalinda;
25. Mwenyezi-Mungu awaangalie kwa wema, na kuwafadhili;
26. Mwenyezi-Mungu awaoneshe wema wake na kuwapa amani.’
27. “Ndivyo watakavyotamka jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.”