Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 6:21-27 Biblia Habari Njema (BHN)

21. “Hiyo ndizo sheria inayomhusu mnadhiri anayeahidi kwa kiapo. Sadaka yake kwa Mwenyezi-Mungu ilingane na nadhiri yake, licha ya chochote kingine anachoweza kutoa; atafanya kulingana na nadhiri aliyoweka, kadiri ya sheria ya kujiweka wakfu kwake.”

22. Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose,

23. “Mwambie Aroni na wanawe kwamba hivi ndivyo mtakavyowabariki Waisraeli: Mtawaambia,

24. ‘Mwenyezi-Mungu awabariki na kuwalinda;

25. Mwenyezi-Mungu awaangalie kwa wema, na kuwafadhili;

26. Mwenyezi-Mungu awaoneshe wema wake na kuwapa amani.’

27. “Ndivyo watakavyotamka jina langu juu ya Waisraeli, nami nitawabariki.”

Kusoma sura kamili Hesabu 6