Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 33:7-18 Biblia Habari Njema (BHN)

7. Kutoka Ethamu, waligeuka na kurudi hadi Pi-hahirothi, mashariki ya Baal-sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.

8. Waliondoka Pi-hahirothi, wakapita bahari ya Shamu mpaka jangwa la Ethamu; walisafiri jangwani mwendo wa siku tatu, wakapiga kambi yao Mara.

9. Kutoka Mara, walisafiri hadi Elimu; huko Elimu kulikuwa na chemchemi kumi na mbili za maji na mitende sabini, wakapiga kambi yao mahali hapo.

10. Walisafiri kutoka Elimu, wakapiga kambi yao karibu na bahari ya Shamu.

11. Kutoka Bahari ya Shamu walipiga kambi yao katika jangwa la Sini.

12. Kutoka jangwa la Sini, walipiga kambi yao Dofka.

13. Kutoka Dofka walipiga kambi yao huko Alushi.

14. Kutoka Alushi walipiga kambi yao huko Refidimu, ambapo hapakuwa na maji ya kunywa.

15. Waliondoka Refidimu wakapiga kambi yao katika jangwa la Sinai.

16. Kutoka Sinai walipiga kambi yao huko Kibroth-hataava.

17. Kutoka Kibroth-hataava, walipiga kambi yao huko Haserothi.

18. Kutoka Haserothi, walipiga kambi yao huko Rithma.

Kusoma sura kamili Hesabu 33