Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 33:29-42 Biblia Habari Njema (BHN)

29. Kutoka Mithka, walipiga kambi yao Hashmona.

30. Kutoka Hashmona, walipiga kambi yao Moserothi.

31. Kutoka Moserothi, walipiga kambi yao Bene-yaakani.

32. Kutoka Bene-yaakani, walipiga kambi yao Hor-hagidgadi.

33. Kutoka Hor-hagidgadi, walipiga kambi yao Yot-batha.

34. Kutoka Yot-batha, walipiga kambi yao Abrona.

35. Kutoka Abrona, walipiga kambi yao Esion-geberi.

36. Waliondoka Esion-geberi, wakasafiri na kupiga kambi yao katika jangwa la Sini, (yaani Kadeshi).

37. Kutoka Kadeshi, walipiga kambi yao mlimani Hori, mpakani mwa nchi ya Edomu.

38. Kwa agizo la Mwenyezi-Mungu kuhani Aroni alipanda juu ya Mlima Hori, na huko, akafariki mnamo siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arubaini tangu Waisraeli walipotoka nchini Misri.

39. Aroni alikuwa na umri wa miaka 123 alipofariki juu ya Mlima Hori.

40. Mfalme wa Aradi, Mkanaani, aliyekaa Negebu katika nchi ya Kanaani, alipata habari kwamba Waisraeli walikuwa wanakuja.

41. Kutoka Mlima Hori, Waisraeli walipiga kambi yao Salmona.

42. Kutoka Salmona, walipiga kambi yao Punoni.

Kusoma sura kamili Hesabu 33