Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 31:43-54 Biblia Habari Njema (BHN)

43. ilikuwa kondoo 337,500,

44. ng'ombe 36,000,

45. punda 30,500,

46. na watu 16,000.

47. Kutoka nusu hii waliyopewa Waisraeli, Mose alitwaa mmoja kati ya kila mateka hamsini na wanyama hamsini, kama alivyoamriwa na Mwenyezi-Mungu, akawapa Walawi ambao walihudumu katika hema la Mwenyezi-Mungu.

48. Kisha maofisa wa majeshi, makapteni na makamanda wa askari wakamwendea Mose,

49. wakamwambia “Watumishi wako tumewahesabu askari wote walio chini yetu na tumeona kwamba hakuna hata mmoja wao anayekosekana.

50. Basi, tumeleta vyombo vya dhahabu, vikuku, bangili, pete za mhuri, vipuli na shanga ambavyo kila mtu alipata. Tumevitoa ili nafsi zetu zifanyiwe upatanisho mbele ya Mwenyezi-Mungu.”

51. Mose na kuhani Eleazari wakapokea vitu vyote vilivyonakshiwa kwa dhahabu.

52. Jumla ya dhahabu yote waliyomtolea Mwenyezi-Mungu ilikuwa karibu kilo 200.

53. (Kila askari alijichukulia nyara zake binafsi).

54. Basi, Mose na kuhani Eleazari wakaipokea dhahabu hiyo kutoka kwa makamanda wakaipeleka katika hema la mkutano, iwe ukumbusho wa Waisraeli mbele ya Mwenyezi-Mungu.

Kusoma sura kamili Hesabu 31