Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 31:32-40 Biblia Habari Njema (BHN)

32. Nyara walizoteka wanajeshi zilikuwa: Kondoo 675,000,

33. ng'ombe 72,000,

34. punda 61,000,

35. na wasichana ambao hawakuwa wamelala na mwanamume 32,000.

36. Nusu yake, sehemu ambayo iligawiwa wanajeshi waliokwenda vitani, ilikuwa kondoo 337,500,

37. katika hao 675 walitolewa kwa Mwenyezi-Mungu.

38. Ngombe wa wanajeshi walikuwa 36,000, na katika hao 72 walitolewa zaka kwa Mwenyezi-Mungu.

39. Punda wao walikuwa 30,500, na katika hao 61 walitolewa zaka kwa Mwenyezi-Mungu.

40. Watu walikuwa 16,000, na katika hao sehemu ya Mwenyezi-Mungu ilikuwa ni watu thelathini na wawili.

Kusoma sura kamili Hesabu 31