Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 31:10-14 Biblia Habari Njema (BHN)

10. Miji yao yote, makazi yao na kambi zao zote waliziteketeza kwa moto.

11. Walichukua nyara zote na mateka yote, ya watu na ya wanyama,

12. wakampelekea Mose na Eleazari, na jumuiya yote ya Waisraeli iliyokuwa kambini katika nchi tambarare za Moabu, ngambo ya Yordani karibu na Yeriko.

13. Mose, kuhani Eleazari, na viongozi wote wa jumuiya ya Waisraeli walitoka kambini, wakaenda kuwalaki wanajeshi.

14. Mose alikasirishwa na maofisa wa jeshi na makamanda waliosimamia makundi ya majeshi 1,000 na makundi ya wanajeshi mamia waliorudi kutoka vitani.

Kusoma sura kamili Hesabu 31