Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 3:8-18 Biblia Habari Njema (BHN)

8. wataangalia na kutunza vyombo vyote vya hema la mkutano na kuwasaidia Waisraeli wanapotoa huduma zao kwenye mahali patakatifu.

9. Walawi utampa Aroni na wazawa wake makuhani; hao wametolewa kati ya Waisraeli wawahudumie kabisa.

10. Utawateua Aroni na wanawe ili waweze kutekeleza huduma zao za ukuhani; lakini kama mtu yeyote mwingine atakaribia, atauawa.”

11. Mwenyezi-Mungu akaendelea kumwambia Mose,

12. “Angalia, sasa nimewateua Walawi miongoni mwa Waisraeli wote, badala ya kila mzaliwa wa kwanza wa kiume kifunguamimba katika kila familia ya Israeli. Walawi ni wangu,

13. kwani kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijiwekea wakfu kila mzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila mzaliwa wa kwanza wa binadamu hata wa mnyama; wao watakuwa wangu. Mimi ndimi Mwenyezi-Mungu.”

14. Baadaye Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose katika jangwa la Sinai,

15. “Wahesabu wana wa Lawi wote kulingana na koo zao na familia zao, kila mwanamume kuanzia watoto wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi.”

16. Basi, Mose akawahesabu kufuatana na neno la Mwenyezi-Mungu, kama alivyomwamuru.

17. Wafuatao ndio waliokuwa wana wa Lawi: Gershoni, Kohathi na Merari.

18. Na haya ndiyo majina ya wana wa Gershoni kwa kufuata familia zao: Libni na Shimei.

Kusoma sura kamili Hesabu 3