Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 27:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mala, Noa, Hogla, Milka na Tirza walikuwa binti zake Selofehadi. Naye Selofehadi alikuwa mwana wa Heferi, mwana wa Gileadi, mwana wa Makiri, mwana wa Manase mwanawe Yosefu.

2. Basi, hao binti wanne walimwendea Mose, wakasimama mbele yake na kuhani Eleazari na viongozi wote wa jumuiya ya Waisraeli, kwenye mlango wa hema la mkutano, wakasema,

3. “Baba yetu alifia jangwani nyikani na bila mtoto yeyote wa kiume.

4. Yeye hakuwa miongoni mwa wafuasi wa Kora waliokusanyika dhidi ya Mwenyezi-Mungu, bali alikufa kutokana na dhambi yake mwenyewe. Kwa nini basi jina la baba yetu lifutwe katika ukoo wake kwa sababu hakuwa na mtoto wa kiume? Tupe urithi pamoja na ndugu zake baba yetu.”

5. Mose akaleta lalamiko lao mbele ya Mwenyezi-Mungu.

6. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,

7. “Wanachosema binti za Selofehadi ni kweli; wape urithi pamoja na ndugu za baba yao, wachukue urithi wake.

8. Kisha waambie Waisraeli kwamba mtu yeyote akifa bila kuacha mtoto wa kiume, urithi wake atapewa binti yake.

9. Ikiwa hana binti, basi urithi huo watapewa ndugu zake wa kiume.

10. Na ikiwa hana ndugu wa kiume, basi urithi wake utawaendea baba zake, wakubwa na wadogo.

Kusoma sura kamili Hesabu 27