Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 26:51-55 Biblia Habari Njema (BHN)

51. Idadi ya wanaume Waisraeli waliohesabiwa ilikuwa 601,730.

52. Kisha Mwenyezi-Mungu alimwambia Mose,

53. “Makabila haya yatagawiwa nchi iwe urithi wao, kulingana na idadi ya majina yao.

54. Kabila kubwa litapewa sehemu yao kubwa na dogo litapewa sehemu yao ndogo. Kila kabila litapewa urithi wake kulingana na idadi ya watu wake.

55. Hata hivyo ugawaji wa nchi utafanywa kwa kura. Kila kabila litarithi kulingana na majina ya ukoo wao.

Kusoma sura kamili Hesabu 26