25. Hizo ndizo koo za Isakari, jumla wanaume 64,300.
26. Kabila la Zebuluni lilikuwa na jamaa za Seredi, wa Eloni na wa Yaleeli.
27. Hizo ndizo koo za Zebuluni, jumla wanaume 60,500.
28. Kabila la Yosefu baba yao Manase na Efraimu.
29. Kabila la Manase lilikuwa na jamaa ya: Makiri, Gileadi.
30. Yezeri, Heleki,
31. Asrieli, Shekemu,
32. Shemida na Heferi.
33. Selofehadi, mwana wa Heferi hakupata watoto wa kiume bali wa kike tu, nao ni Mala, Noa, Hogla, Milka na Tirza.
34. Hizo ndizo koo za Manase, jumla wanaume 52,700.
35. Kabila la Efraimu lilikuwa na jamaa za Shuthela, Bekeri na Tahani.
36. Ukoo wa Erani ulikuwa na jamaa ya Shuthela.
37. Hizo ndizo koo za Efraimu, jumla wanaume 32,500. Zote hizo zilitokana na Yosefu.
38. Kabila la Benyamini lilikuwa na jamaa za Bela, Ashbeli, Ahiramu,
39. Shufamu na Hufamu.