Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 24:17-23 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Ninamwona, atakayekuja, lakini baadaye,namwona, lakini hayuko karibu.Nyota itatokea kwa wazawa wa Yakobo,atatokea mfalme miongoni mwa Waisraeli.Kwa fimbo yake atawachapa viongozi wa Wamoabuatawaangamiza wazawa wote wa Sethi.

18. Edomu itamilikiwa naye,Seiri itakuwa mali yake,Israeli itapata ushindi mkubwa.

19. Mmoja wa wazawa wa Yakobo atatawalanaye atawaangamiza watakaonusurika wa Ari.”

20. Kisha Balaamu akawaangalia Waamaleki, akatoa kauli hii:“Amaleki ni taifa lenye nguvu kuliko yote,lakini mwishoni litaangamia kabisa.”

21. Kisha Balaamu akawaangalia Wakeni, akatoa kauli hii:“Makao yenu ni salama, enyi Wakeni,kama kiota juu kabisa mwambani.

22. Lakini mtateketezwa, enyi Wakeni.Mtachukuliwa mateka na Ashuru mpaka lini?”

23. Tena Balaamu akatoa kauli hii:“Lo! Nani ataishi, Mungu atakapofanya hayo?

Kusoma sura kamili Hesabu 24