Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 24:11-24 Biblia Habari Njema (BHN)

11. Sasa! Nenda zako. Nilikuwa nimekuahidi kukupa zawadi nyingi, lakini Mwenyezi-Mungu hakukujalia kupata zawadi hizo, amekunyima!”

12. Balaamu akamjibu Balaki, “Je, sikuwaambia wajumbe uliowatuma kwangu

13. kwamba hata kama ungenipa nyumba yako imejaa fedha na dhahabu, mimi sitaweza kukiuka agizo la Mwenyezi-Mungu, kwa kufanya jambo lolote, jema au baya kwa hiari yangu mwenyewe? Nilisema, atakachosema Mwenyezi-Mungu ndicho nitakachokisema.

14. “Sasa ninarudi kwa watu wangu, lakini kabla sijaondoka, acha nikuambie mambo ambayo watu hao watawatendea watu wako siku zijazo.”

15. Basi, Balaamu akatamka kauli hii:“Kauli yangu mimi Balaamu mwana wa Beori,kauli ya mtu aliyefumbuliwa macho,

16. kauli ya mtu aliyesikia maneno ya Mungu,na mtu ajuaye maarifa ya Mungu Mkuu,mtu aonaye maono ya Mungu Mwenye Nguvu,mtu anayesujudu, macho wazi.

17. Ninamwona, atakayekuja, lakini baadaye,namwona, lakini hayuko karibu.Nyota itatokea kwa wazawa wa Yakobo,atatokea mfalme miongoni mwa Waisraeli.Kwa fimbo yake atawachapa viongozi wa Wamoabuatawaangamiza wazawa wote wa Sethi.

18. Edomu itamilikiwa naye,Seiri itakuwa mali yake,Israeli itapata ushindi mkubwa.

19. Mmoja wa wazawa wa Yakobo atatawalanaye atawaangamiza watakaonusurika wa Ari.”

20. Kisha Balaamu akawaangalia Waamaleki, akatoa kauli hii:“Amaleki ni taifa lenye nguvu kuliko yote,lakini mwishoni litaangamia kabisa.”

21. Kisha Balaamu akawaangalia Wakeni, akatoa kauli hii:“Makao yenu ni salama, enyi Wakeni,kama kiota juu kabisa mwambani.

22. Lakini mtateketezwa, enyi Wakeni.Mtachukuliwa mateka na Ashuru mpaka lini?”

23. Tena Balaamu akatoa kauli hii:“Lo! Nani ataishi, Mungu atakapofanya hayo?

24. Meli zitafika kutoka Kitimu,wataishambulia Ashuru na Eberi,lakini nao pia wataangamia milele.”

Kusoma sura kamili Hesabu 24