Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 24:1-8 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Sasa Balaamu alitambua kwamba Mwenyezi-Mungu alipenda kuwabariki Waisraeli, kwa hiyo hakwenda kupiga bao tena, akawa anaangalia jangwani.

2. Alitazama juu akawaona Waisraeli wamepiga kambi, kila kabila mahali pake. Kisha roho ya Mungu ikamjia,

3. naye akatamka kauli hii ya kinabii:Kauli yangu mimi Balaamu mwana wa Peorikauli ya mtu aliyefumbuliwa macho;

4. kauli ya mtu aliyesikia maneno ya Mungumtu aliyeona maono ya Mungu Mwenye Nguvu,mtu anayesujudu na kuona wazi.

5. Hema zako zapendeza namna gani enyi watu wa Yakobo;naam, kambi zenu enyi watu wa Israeli!

6. Ni kama mabonde yanayotiririka maji,kama bustani kandokando ya mto,kama mishubiri aliyopanda Mwenyezi-Mungu,kama mierezi kandokando ya maji.

7. Watakuwa na hazina ya kutosha ya maji,mbegu yao itapata maji mengi,mfalme wao atakuwa mkuu kuliko Agagi,na ufalme wake utatukuka sana.

8. Mungu aliwachukua kutoka Misri,naye huwapigania kwa nguvu kama nyati.Atayateketeza mataifa yaliyo adui zao,atavunjavunja mifupa yao,atawachoma kwa mishale yake.

Kusoma sura kamili Hesabu 24