Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 23:20-26 Biblia Habari Njema (BHN)

20. Tazama, nimepewa amri ya kubariki,naye amebariki wala siwezi kuitangua.

21. Mwenyezi-Mungu hajaona ubaya kwa wana wa Yakobo,wala udhia kwa hao wana wa Israeli.Mwenyezi-Mungu Mungu wao yuko pamoja nao,Yeye husifiwa kwa vifijo miongoni mwao,yeye huzipokea sifa zao za kifalme.

22. Mungu aliyewachukua kutoka Misri,huwapigania kwa nguvu kama za nyati.

23. Hakika ulozi hauwezi kuwapinga watu wa Yakobo,wala uchawi dhidi ya watu wa Israeli.Sasa kuhusu Israeli, watu watasema,‘Tazameni maajabu aliyotenda Mungu!’

24. Tazama! Waisraeli wameinuka kama simba jike,wanasimama kama simba dume.Ni kama simba asiyelala mpaka amalize mawindo yake,na kunywa damu ya mawindo.”

25. Ndipo Balaki akamwambia Balaamu, “Basi, usiwalaani wala usiwabariki kabisa!”

26. Lakini Balaamu akamjibu Balaki, “Je, sikukuambia kwamba anachosema Mwenyezi-Mungu ndicho ninachopaswa kufanya?”

Kusoma sura kamili Hesabu 23