Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 22:38-41 Biblia Habari Njema (BHN)

38. Balaamu akamjibu Balaki, “Sasa nimekuja! Lakini, je, nina mamlaka ya kusema chochote tu? Jambo atakaloniambia Mungu ndilo ninalopaswa kusema.”

39. Basi, Balaamu akaenda pamoja na Balaki wakafika mjini Kiriath-husothi.

40. Huko Balaki alitoa kafara ya ng'ombe na kondoo, akawagawia nyama Balaamu na maofisa waliokuwa pamoja naye.

41. Kesho yake, Balaki alimchukua Balaamu, akapanda naye mpaka Bamoth-baali; kutoka huko, Balaamu aliweza kuwaona baadhi ya Waisraeli.

Kusoma sura kamili Hesabu 22