Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 21:17-30 Biblia Habari Njema (BHN)

17. Hapo Waisraeli waliimba wimbo huu:“Bubujika maji ee kisima! – Kiimbieni!

18. Kisima kilichochimbwa na wakuukilichochimbwa sana na wenye cheo,kwa fimbo zao za enzi na bakora.”Kutoka jangwani walisafiri mpaka Matana,

19. kutoka Matana mpaka Nahalieli, kutoka Nahalieli mpaka Bamothi,

20. na kutoka Bamothi mpaka kwenye bonde linaloingia nchi ya Moabu, kwenye kilele cha Mlima Pisga, kielekeacho chini jangwani.

21. Waisraeli walimpelekea mfalme Sihoni wa Waamori, ujumbe huu:

22. “Turuhusu tupite katika nchi yako; hatutakwenda pembeni na kuingia mashambani au katika mashamba ya mizabibu, wala hatutakunywa maji ya visima vyenu; tutapita moja kwa moja katika barabara kuu ya mfalme mpaka tumeondoka nchini mwako.”

23. Lakini Sihoni hakuwaruhusu watu wa Israeli wapite katika nchi yake. Aliwakusanya watu wake, akaenda Yahasa Jangwani kuwashambulia Waisraeli.

24. Lakini Waisraeli walimuua, wakaitwaa nchi yake tangu mto Arnoni hadi mto Yaboki, yaani hadi mpaka wa nchi ya Waamoni ambao ulikuwa unalindwa sana.

25. Waisraeli waliiteka miji hii yote nao wakaishi katika miji ya Waamori katika Heshboni na vitongoji vyake.

26. Heshboni ulikuwa mji wa Sihoni mfalme wa Waamori, ambaye hapo awali alikuwa amepigana na mfalme wa Moabu na kuiteka nchi yake yote mpaka mto Arnoni.

27. Ndiyo maana washairi wetu huimba:“Njoni Heshboni na kujenga.Mji wa Sihoni na ujengwe na kuimarishwa.

28. Maana moto ulitoka Heshboni,miali ya moto ilitoka mjini kwa Sihoni,uliuteketeza mji wa Ari wa Moabu,ukaiangamiza milima ya mto Arnoni.

29. Ole wenu watu wa Moabu!Mmeangamizwa, enyi watu wa mungu Kemoshi!Umewafanya watoto wenu wa kiume kuwa wakimbizi,binti zako umewaacha wachukuliwe matekampaka kwa Sihoni, mfalme wa Amori.

30. Lakini sasa wazawa wao wameangamizwa,kutoka Heshboni mpaka Diboni,kutoka Nashimu mpaka Nofa, karibu na Medeba.”

Kusoma sura kamili Hesabu 21