Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 16:22-25 Biblia Habari Njema (BHN)

22. Lakini Mose na Aroni wakajitupa chini kifudifudi na kusema, “Ee Mwenyezi-Mungu uliye asili ya uhai wa binadamu wote. Je, mtu mmoja akikukosea, utaikasirikia jumuiya nzima?”

23. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,

24. “Waambie watu waondoke karibu na makao ya hema ya Kora, Dathani na Abiramu.”

25. Basi, Mose akaenda kwa Dathani na Abiramu, akifuatwa na wazee wa Israeli.

Kusoma sura kamili Hesabu 16