22. Lakini Mose na Aroni wakajitupa chini kifudifudi na kusema, “Ee Mwenyezi-Mungu uliye asili ya uhai wa binadamu wote. Je, mtu mmoja akikukosea, utaikasirikia jumuiya nzima?”
23. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,
24. “Waambie watu waondoke karibu na makao ya hema ya Kora, Dathani na Abiramu.”
25. Basi, Mose akaenda kwa Dathani na Abiramu, akifuatwa na wazee wa Israeli.