Agano la Kale

Agano Jipya

Hesabu 13:1-12 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mwenyezi-Mungu akamwambia Mose,

2. “Tuma watu waende wakaipeleleze nchi ya Kanaani ambayo ninawapa wana wa Israeli. Utatuma mtu mmoja kutoka katika kila kabila, na mtu huyo lazima awe kiongozi katika kabila lake.”

3. Basi, kwa mujibu wa agizo la Mwenyezi-Mungu, Mose akatuma watu kutoka jangwa la Parani. Watu wote waliotumwa walikuwa viongozi wa makabila mbalimbali ya wana wa Israeli.

4. Ifuatayo ndiyo orodha ya majina ya watu hao:Kabila la Reubeni, Shamua mwana wa Zakuri.

5. Kabila la Simeoni, Shafati mwana wa Hori.

6. Kabila la Yuda, Kalebu mwana wa Yefune.

7. Kabila la Isakari, Igali mwana wa Yosefu.

8. Kabila la Efraimu, Hoshea mwana wa Nuni.

9. Kabila la Benyamini, Palti mwana wa Rafu.

10. Kabila la Zebuluni, Gadieli mwana wa Sodi.

11. Kabila la Yosefu (yaani kabila la Manase), Gadi mwana wa Susi.

12. Kabila la Dani, Amieli mwana wa Gemali.

Kusoma sura kamili Hesabu 13