Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 2:4-13 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Andika:‘Waangalie wenye kiburi, hao wataangamia;lakini waadilifu wataishi kwa kumwamini Mungu.’”

5. Zaidi ya hayo, divai hupotosha;mtu mwenye kiburi hatadumu.Yuko tayari kuwameza wengine kama Kuzimu;kama vile kifo, hatosheki na kitu.Hujikusanyia mataifa yote,na watu wote kama mali yake.

6. Kila mtu atamdhihaki mtu wa namna hiyona kumtungia misemo ya dhihaka:“Ole wako unayejirundikia visivyo vyako,na kuchukua rehani mali za watu lakini hulipi!Utaendelea kufanya hivyo hadi lini?

7. Siku moja wadeni wako watainuka ghafla,wale wanaokutetemesha wataamka.Ndipo utakuwa mateka wao.

8. Wewe umeyapora mataifa mengi,lakini wote wanaosalimika watakupora wewe,kwa mauaji na dhuluma uliyoitendea dunia,naam, uliyoifanyia miji na wakazi wake wote.

9. “Ole wako unayejitajirisha kwa hasara ya mwingine,ujengaye nyumba yako juu milimaniukidhani kuwa salama mbali na madhara.

10. Lakini kwa mipango yako umeiaibisha jamaa yako.Kwa kuyaangamiza mataifa mengi,umeyaangamiza maisha yako mwenyewe.

11. Ndiyo maana hata mawe yatalalamika ukutani,na boriti za nyumba zitayaunga mkono.

12. “Ole wako unayejenga mji kwa mauajiunayesimika jiji kwa maovu!

13. Mwenyezi-Mungu wa majeshi husababishajuhudi za watu zipotelee motoni,na mataifa yajishughulishe bure.

Kusoma sura kamili Habakuki 2