Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 2:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia,na kukaa juu mnarani;nitakaa macho nione ataniambia nini,atajibu nini kuhusu lalamiko langu.”

2. Kisha, Mwenyezi-Mungu akanijibu hivi:“Yaandike maono haya;yaandike wazi juu ya vibao,anayepitia hapo apate kuyasoma.

3. Maono haya yanangoja wakati wa kufaa;ni maono ya ukweli juu ya mwisho.Kama yaonekana kuchelewa, uyasubiri;hakika yatafika, wala hayatachelewa.

4. Andika:‘Waangalie wenye kiburi, hao wataangamia;lakini waadilifu wataishi kwa kumwamini Mungu.’”

5. Zaidi ya hayo, divai hupotosha;mtu mwenye kiburi hatadumu.Yuko tayari kuwameza wengine kama Kuzimu;kama vile kifo, hatosheki na kitu.Hujikusanyia mataifa yote,na watu wote kama mali yake.

6. Kila mtu atamdhihaki mtu wa namna hiyona kumtungia misemo ya dhihaka:“Ole wako unayejirundikia visivyo vyako,na kuchukua rehani mali za watu lakini hulipi!Utaendelea kufanya hivyo hadi lini?

7. Siku moja wadeni wako watainuka ghafla,wale wanaokutetemesha wataamka.Ndipo utakuwa mateka wao.

Kusoma sura kamili Habakuki 2