1. Mimi nitasimama mahali pa kuchungulia,na kukaa juu mnarani;nitakaa macho nione ataniambia nini,atajibu nini kuhusu lalamiko langu.”
2. Kisha, Mwenyezi-Mungu akanijibu hivi:“Yaandike maono haya;yaandike wazi juu ya vibao,anayepitia hapo apate kuyasoma.
3. Maono haya yanangoja wakati wa kufaa;ni maono ya ukweli juu ya mwisho.Kama yaonekana kuchelewa, uyasubiri;hakika yatafika, wala hayatachelewa.
4. Andika:‘Waangalie wenye kiburi, hao wataangamia;lakini waadilifu wataishi kwa kumwamini Mungu.’”
5. Zaidi ya hayo, divai hupotosha;mtu mwenye kiburi hatadumu.Yuko tayari kuwameza wengine kama Kuzimu;kama vile kifo, hatosheki na kitu.Hujikusanyia mataifa yote,na watu wote kama mali yake.
6. Kila mtu atamdhihaki mtu wa namna hiyona kumtungia misemo ya dhihaka:“Ole wako unayejirundikia visivyo vyako,na kuchukua rehani mali za watu lakini hulipi!Utaendelea kufanya hivyo hadi lini?
7. Siku moja wadeni wako watainuka ghafla,wale wanaokutetemesha wataamka.Ndipo utakuwa mateka wao.