Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 1:9-17 Biblia Habari Njema (BHN)

9. “Wote wanakuja kufanya ukatili;kwa nyuso kakamavu wanasonga mbele,wanakusanya mateka wengi kama mchanga.

10. Wanawadhihaki wafalme,na kuwadharau watawala.Kila ngome kwao ni mzaha,wanairundikia udongo na kuiteka.

11. Kisha wanasonga mbele kama upepo,wafanya makosa na kuwa na hatia,maana, nguvu zao ndizo mungu wao!”

12. “Je, wewe si ndiwe Mwenyezi-Mungu,tangu kale na kale?Wewe ndiwe Mungu wangu, Mtakatifu wangu, usiyekufaEe Mwenyezi-Mungu, umewateua Wakaldayo watuhukumu;Ewe Mwamba, umewaimarisha ili watuadhibu!

13. Wewe ni mtakatifu kabisa, huwezi kutazama uovu,huwezi kustahimili kamwe kuona mabaya.Mbona basi wawaona wafanya maovu na kunyamaza,kwa nini unanyamaza waovu wanapowamalizawale watu walio waadilifu kuliko wao?

14. “Umewafanya watu kama samaki baharini,kama viumbe vitambaavyo visivyo na kiongozi!

15. Wakaldayo huwavua watu kwa ndoana,huwavutia nje kwa wavu wao,huwakusanya wote katika jarife lao,kisha hufurahi na kushangilia.

16. Kwa hiyo, wanazitambikia nyavu zao,na kuzifukizia ubani;maana kwa hizo huweza kuishi kwa anasa,na kula chakula cha fahari.

17. “Je, hawataacha kamwe kuvuta upinde wao?Je, wataendelea tu kuwanasa watu,na kuyaangamiza mataifa bila huruma?

Kusoma sura kamili Habakuki 1