Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 1:3-10 Biblia Habari Njema (BHN)

3. Kwa nini wanifanya nishuhudie mabaya na taabu?Uharibifu na ukatili vinanizunguka,ugomvi na mashindano yanazuka.

4. Hivyo sheria haina nguvu,wala haki haitekelezwi.Waovu wanawazunguka waadilifu,hivyo hukumu hutolewa ikiwa imepotoshwa.”

5. Mungu akasema:“Yaangalie mataifa, uone!Utastaajabu na kushangaa.Maana ninatenda kitu ukiwa bado unaishi,kitu ambacho ungeambiwa hungesadiki.

6. Maana ninawachochea Wakaldayo,taifa lile kali na lenye hamaki!Taifa lipitalo katika nchi yote,ili kunyakua makao ya watu wengine.

7. Wao ni watu wa kuchukiza na kutisha;wao hujiamulia wenyewe nini haki na adhama.

8. “Farasi wao ni wepesi kuliko chui;wakali kuliko mbwamwitu wenye njaa.Wapandafarasi wao wanatoka mbali,wanaruka kasi kama tai arukiavyo mawindo.

9. “Wote wanakuja kufanya ukatili;kwa nyuso kakamavu wanasonga mbele,wanakusanya mateka wengi kama mchanga.

10. Wanawadhihaki wafalme,na kuwadharau watawala.Kila ngome kwao ni mzaha,wanairundikia udongo na kuiteka.

Kusoma sura kamili Habakuki 1