Agano la Kale

Agano Jipya

Habakuki 1:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Kauli ya Mungu aliyoiona nabii Habakuki.

2. “Ee Mwenyezi-Mungu, nitakulilia mpaka lini,nawe usinisikilize na kunisaidia?Kwa nini nalia: ‘Dhuluma’nawe hutuokoi?

3. Kwa nini wanifanya nishuhudie mabaya na taabu?Uharibifu na ukatili vinanizunguka,ugomvi na mashindano yanazuka.

4. Hivyo sheria haina nguvu,wala haki haitekelezwi.Waovu wanawazunguka waadilifu,hivyo hukumu hutolewa ikiwa imepotoshwa.”

Kusoma sura kamili Habakuki 1