Agano la Kale

Agano Jipya

Ezra 4:21-24 Biblia Habari Njema (BHN)

21. Kwa hiyo, toeni amri watu hao waache kuujenga upya mji huo hadi hapo nitakapotoa maagizo mengine.

22. Tena, angalieni sana msichelewe kufanya hivyo, nisije nikapata hasara.”

23. Mara tu waliposomewa barua hii kutoka kwa Artashasta, Rehumu, katibu Shimshai na wenzao waliharakisha kwenda Yerusalemu na kuwalazimisha kwa nguvu Wayahudi waache kuujenga mji.

24. Kazi ya kuijenga upya nyumba ya Mungu mjini Yerusalemu ilisimama, na hali hiyo iliendelea mpaka mwaka wa pili wa utawala wa Dario, mfalme wa Persia.

Kusoma sura kamili Ezra 4