Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 7:9-14 Biblia Habari Njema (BHN)

9. Sitawaachilia wala sitawaonea huruma.Nitawaadhibu kulingana na mienendo yenumaadamu machukizo yapo bado miongoni mwenu.Ndipo mtakapotambua kuwa ni mimi Mwenyezi-Mungu ninayewaangamiza.

10. “Tazameni, siku ile inakuja!Maangamizi yenu yamekuja.Ukatili uko kila mahali na kiburi kimechanua.

11. Ukatili unaendelea kuwa mbaya zaidi.Hakuna hata mmoja wenu atakayebaki,wala vitu mlivyojirundikia kwa wingi au utajiri wenu;hatakuwako mtu mwenye heshima miongoni mwenu.

12. Wakati umewadia,naam, ile siku imekaribia.Mnunuzi asifurahi wala mwuzaji asiomboleze;kwa sababu ghadhabu yangu itaukumba umati wote.

13. Wauzaji hawataweza kurudia mali yao waliyouzahata kama wakibaki hai.Kwani maono haya yahusu umati wote na hayatabatilishwa.Kutokana na uovu huo, hakuna mtu atakayesalimisha maisha yake.

14. Tarumbeta imepigwa na kuwafanya wote wawe tayari.Lakini hakuna anayekwenda vitani,kwani ghadhabu yangu iko juu ya umati wote.

Kusoma sura kamili Ezekieli 7