Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 7:1-13 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Wewe mtu, waambie wakazi wa nchi ya Israeli kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Sasa ni mwisho!Mwisho umeifikia nchi yote kutoka pande zote nne!

3. Sasa mwisho umewafikia;sasa mtausikia ukali wa hasira yangu juu yenu.Nitawahukumu kadiri ya mwenendo wenu.Nitawaadhibu kwa machukizo yenu yote.

4. Sitawaachia wala sitawahurumia;nitawaadhibu kulingana na mienendo yenu,maadamu machukizo bado yapo kati yenu.Ndipo mtakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.

5. Ninachosema mimi Bwana Mwenyezi-Mungu ni hiki:Mtapatwa na maafa mfululizo!

6. Mwisho umekuja!Naam, mwisho umefika!Umewafikia nyinyi!

7. Enyi wakazi wa nchi hii, maangamizi yenu yamewajia!Wakati umekuja;naam, siku imekaribia.Hiyo ni siku ya msukosukona siyo ya sauti za shangwe mlimani.

8. Sasa mtausikia uzito wa hasira yangu juu yenu.Nitawahukumu kulingana na mwenendo wenu;nitawaadhibu kadiri ya machukizo yenu.

9. Sitawaachilia wala sitawaonea huruma.Nitawaadhibu kulingana na mienendo yenumaadamu machukizo yapo bado miongoni mwenu.Ndipo mtakapotambua kuwa ni mimi Mwenyezi-Mungu ninayewaangamiza.

10. “Tazameni, siku ile inakuja!Maangamizi yenu yamekuja.Ukatili uko kila mahali na kiburi kimechanua.

11. Ukatili unaendelea kuwa mbaya zaidi.Hakuna hata mmoja wenu atakayebaki,wala vitu mlivyojirundikia kwa wingi au utajiri wenu;hatakuwako mtu mwenye heshima miongoni mwenu.

12. Wakati umewadia,naam, ile siku imekaribia.Mnunuzi asifurahi wala mwuzaji asiomboleze;kwa sababu ghadhabu yangu itaukumba umati wote.

13. Wauzaji hawataweza kurudia mali yao waliyouzahata kama wakibaki hai.Kwani maono haya yahusu umati wote na hayatabatilishwa.Kutokana na uovu huo, hakuna mtu atakayesalimisha maisha yake.

Kusoma sura kamili Ezekieli 7