Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 39:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Nitakugeuza na kukuelekeza upande mwingine na kukuongoza kutoka mbali kaskazini uende kushambulia milima ya Israeli.

3. Kisha nitauvunja upinde wako katika mkono wako wa kushoto, na mishale yako katika mkono wako wa kulia nitaiangusha chini.

4. Utakufa juu ya milima ya Israeli, wewe pamoja na vikosi vyako vyote na mataifa yaliyo pamoja nawe. Nami nitaitoa miili yao iliwe na ndege wa kila aina na wanyama wakali.

5. Utafia porini. Mimi Mwenyezi-Mungu nimesema.

6. Nitapeleka moto juu ya Magogu na juu ya wote wakaao salama katika nchi za pwani. Nao watatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.

7. Nitalifanya jina langu takatifu litambuliwe na watu wangu Israeli, wala sitaruhusu tena watu walikufuru jina langu takatifu. Nayo mataifa yatatambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu, Mtakatifu wa Israeli.

8. “Siku ile ninayosema juu yake kwa hakika inakuja. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.

Kusoma sura kamili Ezekieli 39