Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 38:18-23 Biblia Habari Njema (BHN)

18. Bwana Mwenyezi-Mungu asema hivi: “Siku ile Gogu atakapoishambulia nchi ya Israeli, nitawasha ghadhabu yangu.

19. Mimi natamka rasmi kwa wivu na ghadhabu yangu kali kwamba siku hiyo kutakuwa na tetemeko kubwa la ardhi nchini Israeli.

20. Samaki baharini na ndege warukao, wanyama wa porini, viumbe vyote vitambaavyo pamoja na watu wote duniani, watatetemeka kwa kuniona. Milima itaporomoshwa, magenge yataanguka na kuta zote zitaanguka chini.

21. Nami nitasababisha kila namna ya tisho kumkabili Gogu. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema. Wanajeshi wake wataanza kushambuliana wenyewe kwa mapanga yao.

22. Nitamwadhibu Gogu kwa magonjwa mabaya na mauaji. Nitanyesha mvua nyingi, mvua ya mawe na moto wa madini ya kiberiti juu yake, juu ya vikosi vyake, na mataifa yale mengi yaliyo pamoja naye.

23. Ndivyo nitakavyofanya mataifa yote yaone ukuu wangu na utakatifu wangu. Ndipo watakapotambua kuwa mimi ni Mwenyezi-Mungu.”

Kusoma sura kamili Ezekieli 38