Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 28:1-6 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Wewe mtu! Mwambie mfalme wa Tiro kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Wewe una kiburi cha moyo,na umesema kwamba wewe ni mungu,kwamba umekalia kiti cha enzi cha miungu,umekaa mbali huko baharini.Lakini, wewe ni binadamu tu wala si Mungu,ingawa wajiona kuwa una hekima kama Mungu.

3. Haya! Wewe wajiona mwenye hekima kuliko Danieli,wadhani hakuna siri yoyote usiyoijua.

4. Kwa hekima na akili yakoumejipatia utajiri,umejikusanyia dhahabu na fedhaukaziweka katika hazina zako.

5. Kwa busara yako kubwa katika biasharaumejiongezea utajiri wako,ukawa na kiburi kwa mali zako!

6. Kwa hiyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Kwa vile unajiona mwenye hekima kama Mungu,

Kusoma sura kamili Ezekieli 28