Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 28:1-10 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Wewe mtu! Mwambie mfalme wa Tiro kuwa mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Wewe una kiburi cha moyo,na umesema kwamba wewe ni mungu,kwamba umekalia kiti cha enzi cha miungu,umekaa mbali huko baharini.Lakini, wewe ni binadamu tu wala si Mungu,ingawa wajiona kuwa una hekima kama Mungu.

3. Haya! Wewe wajiona mwenye hekima kuliko Danieli,wadhani hakuna siri yoyote usiyoijua.

4. Kwa hekima na akili yakoumejipatia utajiri,umejikusanyia dhahabu na fedhaukaziweka katika hazina zako.

5. Kwa busara yako kubwa katika biasharaumejiongezea utajiri wako,ukawa na kiburi kwa mali zako!

6. Kwa hiyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Kwa vile unajiona mwenye hekima kama Mungu,

7. basi nitakuletea watu wageni,mataifa katili kuliko yote.Wataharibu fahari ya hekima yakona kuchafua uzuri wako.

8. Watakutumbukiza chini shimoni,nawe utakufa kifo cha kikatili kilindini mwa bahari.

9. Je, utajiona bado kuwa mungumbele ya hao watakaokuua?Mikononi mwa hao watakaokuangamiza,utatambua kuwa wewe ni mtu tu, wala si Mungu!

10. Utakufa kifo cha aibu kubwamikononi mwa watu wa mataifa.Ni mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.”

Kusoma sura kamili Ezekieli 28