Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 23:28-39 Biblia Habari Njema (BHN)

28. “Naam, mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Nitakutia mikononi mwa watu unaowachukia, watu unaowaona kuwa kinyaa.

29. Na, kwa vile wanakuchukia, watakunyanganya matunda yote ya kazi yako na kukuacha uchi, bila nguo na kuonesha aibu ya uzinzi wako. Uzinzi wako na uasherati wako

30. ndivyo vilivyokuletea hali hiyo. Wewe ulizini na mataifa, ukajitia najisi kwa miungu yao.

31. Kwa kuwa ulifuata nyayo za dada yako, basi, mimi nitakupa kikombe kilekile cha adhabu ukinywe.

32. “Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi:Utakunywa toka kikombe cha dada yako;kikombe kikubwa na cha kina kirefu.Watu watakucheka na kukudharau;na kikombe chenyewe kimejaa.

33. Kitakulewesha na kukuhuzunisha sana.Kikombe cha dada yako Samaria,ni kikombe cha hofu na maangamizi.

34. Utakinywa na kukimaliza kabisa;utakipasua vipandevipande kwa meno,na kurarua navyo matiti yako.Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.

35. “Kwa hiyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi: Kwa kuwa umenisahau na kunipa kisogo, basi, utawajibika kwa uasherati na uzinzi wako.”

36. Mwenyezi-Mungu aliniambia, “Wewe mtu! Je, uko tayari kuwahukumu Ohola na Oholiba? Basi, watangazie matendo yao ya kuchukiza!

37. Wamefanya uzinzi na mauaji. Wamefanya ukahaba kwa sanamu zao, hata kuzitambikia watoto walionizalia wao wenyewe.

38. Tena si hayo tu! Wameikufuru maskani yangu na kuzitangua sabato zangu.

39. Siku ileile walipozitambikia sanamu watoto wao wenyewe, waliingia patakatifu ili wapatie unajisi. Hayo ndiyo waliyoyafanya nyumbani mwangu.

Kusoma sura kamili Ezekieli 23