Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 22:6-11 Biblia Habari Njema (BHN)

6. “Wakuu wa Israeli walioko kwako, kila mmoja kadiri ya nguvu zake huua watu.

7. Kwako baba na mama wanadharauliwa. Mgeni anayekaa kwako anapokonywa mali yake. Yatima na wajane wanaonewa.

8. Wewe umedharau vyombo vyangu vitakatifu na kuzikufuru sabato zangu.

9. Kwako wamo wanaowasingizia wengine ili wauawe. Wakazi wako hushiriki chakula kilichotolewa kwa miungu milimani. Watu wako wanatenda ufisadi.

10. Kwako wamo watu ambao hulala na wake za baba zao. Huwanajisi wanawake katika siku zao za hedhi.

11. Wengine hufanya machukizo kwa kulala na wake za majirani zao. Wengine hulala na wake za watoto wao, na wengine hulala na dada zao.

Kusoma sura kamili Ezekieli 22