Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 2:1-5 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Naye akaniambia, “Wewe mtu! Simama wima. Nataka kuongea nawe.”

2. Alipokuwa akiongea nami, roho ya Mungu ikaniingia na kunisimamisha wima. Ndipo nikamsikia

3. akiniambia, “Wewe mtu nakutuma kwa Waisraeli, taifa la waasi ambao wameniasi. Wameendelea kunikosea mimi hadi leo kama walivyokuwa wazee wao.

4. Watu hao ni wafidhuli na wajeuri. Nakutuma kwao, nawe utawaambia kwamba mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema hivi na hivi.

5. Wakisikia au wasiposikia, maana wao ni watu waasi, walau watatambua kwamba nabii amekuwapo miongoni mwao.

Kusoma sura kamili Ezekieli 2