Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 19:4-8 Biblia Habari Njema (BHN)

4. Mataifa yakapiga mbiu ya hatari dhidi yake,wakamnasa katika mtego wao,wakampeleka kwa ndoana mpaka Misri.

5. Mama yake alipoona kuwa amechoka kungoja,matumaini ya kumpata yamekwisha,alimchukua mtoto wake mwingine,akamfanya simba kijana hodari.

6. Huyo alipokuwa amekua,akaanza kuzurura na simba wengine.Naye pia akajifunza kuwinda,akawa simba mla watu.

7. Aliziandama ngome za watuna kuiharibu miji yao.Nchi ikatishika pamoja na wakazi wake,kwa sauti ya kunguruma kwake.

8. Mataifa yakamkabili kutoka mkoani mwao kote,wakatandaza wavu wao juu yake,naye akanaswa katika mtego wao.

Kusoma sura kamili Ezekieli 19