Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 18:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Kwa nini mnarudiarudia methali hii katika nchi ya Israeli:‘Akina baba wamekula zabibu mbichi,lakini meno ya watoto wao yakatiwa ganzi!’

3. Lakini, kama niishivyo mimi Bwana Mwenyezi-Mungu, nasema kwamba methali hii haitatumika tena katika Israeli.

4. Jueni kwamba uhai wote ule ni wangu, uhai wa mzazi na uhai wa mtoto. Yeyote anayetenda dhambi, ndiye atakayekufa.

5. “Kama mtu ni mwadilifu, anafuata yaliyo haki na sawa,

6. kama hashiriki tambiko za sanamu za miungu mlimani wala kuzitegemea sanamu za miungu ya Waisraeli, kama hatembei na mke wa jirani yake wala kulala na mwanamke wakati wa siku zake,

7. kama hamdhulumu mtu yeyote, bali hurudisha rehani, kama hanyanganyi watu mali zao, bali huwapa chakula wenye njaa na kuwavalisha walio uchi,

Kusoma sura kamili Ezekieli 18