Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 13:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

2. “Wewe mtu, wakaripie manabii wa Israeli wanaotangaza mambo ambayo wameyafikiria wao wenyewe. Waambie wasikilize yale ambayo mimi Mwenyezi-Mungu ninasema.

3. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema: Ole wenu manabii wapumbavu mnaofuata mawazo yenu wenyewe na maono yenu wenyewe!

4. Manabii wenu, enyi Waisraeli ni kama mbweha wanaopitapita katika magofu.

Kusoma sura kamili Ezekieli 13