1. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:
2. “Wewe mtu, wakaripie manabii wa Israeli wanaotangaza mambo ambayo wameyafikiria wao wenyewe. Waambie wasikilize yale ambayo mimi Mwenyezi-Mungu ninasema.
3. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema: Ole wenu manabii wapumbavu mnaofuata mawazo yenu wenyewe na maono yenu wenyewe!
4. Manabii wenu, enyi Waisraeli ni kama mbweha wanaopitapita katika magofu.