Agano la Kale

Agano Jipya

Ezekieli 12:24-28 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Maana hapatakuwa tena na maono ya uongo au kupiga bao miongoni mwa Waisraeli.

25. Mimi Mwenyezi-Mungu mwenyewe nitatangaza yatakayotukia. Nayo yatatukia bila kukawia. Wakati wa uhai wenu, enyi watu waasi, neno nitakalotamka nitalitimiza. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema.”

26. Neno la Mwenyezi-Mungu lilinijia:

27. “Wewe mtu, Waisraeli wanafikiri kwamba maono yako yanahusu siku za baadaye sana, na unabii wako wahusu nyakati za mbali sana!

28. Kwa hiyo waambie, kwamba mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nasema kuwa maneno yangu yote yatatimia karibuni. Mimi Bwana Mwenyezi-Mungu nimesema!”

Kusoma sura kamili Ezekieli 12