Agano la Kale

Agano Jipya

Esta 1:1-4 Biblia Habari Njema (BHN)

1. Mfalme Ahasuero, alipotawala ufalme wake ulikuwa mikoa 127, toka India hadi Kushi.

2. Kiti chake cha enzi kilikuwa katika mji mkuu Susa.

3. Mnamo mwaka wa tatu wa utawala wake, mfalme Ahasuero aliwaandalia karamu viongozi na watumishi wake wa serikali, wakuu wa majeshi ya Persia na Media, watu maarufu na wakuu wa mikoa.

4. Basi, kwa muda wa miezi sita, Ahasuero akaonesha utajiri wa ufalme wake mtukufu, na fahari ya utawala wake.

Kusoma sura kamili Esta 1