Agano la Kale

Agano Jipya

Danieli 6:25-28 Biblia Habari Njema (BHN)

25. Ndipo mfalme Dario akawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote, na lugha zote duniani:“Nawatakieni amani kwa wingi.

26. Nitatoa amri kwamba watu wote katika ufalme wangu ni lazima wamwogope na kumcha Mungu wa Danieli.“Yeye ni Mungu aliye hai, aishiye milele;ufalme wake kamwe hauwezi kuangamizwa,utawala wake hauna mwisho.

27. Yeye hukomboa na kuokoa,hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani,maana amemwokoa Danieli makuchani mwa simba.”

28. Basi, Danieli akapata fanaka wakati wa utawala wa mfalme Dario na wa mfalme Koreshi, Mpersi.

Kusoma sura kamili Danieli 6