Agano la Kale

Agano Jipya

Danieli 6:24-28 Biblia Habari Njema (BHN)

24. Mfalme akaamuru wale watu waliomchongea Danieli wakamatwe, nao wakatupwa ndani ya lile pango la simba pamoja na wake zao na watoto wao. Nao, hata kabla hawajagusa chini, simba waliwashambulia na kuivunjavunja mifupa yao.

25. Ndipo mfalme Dario akawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote, na lugha zote duniani:“Nawatakieni amani kwa wingi.

26. Nitatoa amri kwamba watu wote katika ufalme wangu ni lazima wamwogope na kumcha Mungu wa Danieli.“Yeye ni Mungu aliye hai, aishiye milele;ufalme wake kamwe hauwezi kuangamizwa,utawala wake hauna mwisho.

27. Yeye hukomboa na kuokoa,hufanya ishara na maajabu mbinguni na duniani,maana amemwokoa Danieli makuchani mwa simba.”

28. Basi, Danieli akapata fanaka wakati wa utawala wa mfalme Dario na wa mfalme Koreshi, Mpersi.

Kusoma sura kamili Danieli 6