Agano la Kale

Agano Jipya

Danieli 4:1-7 Biblia Habari Njema (BHN)

1. “Mimi mfalme Nebukadneza, nawaandikia watu wa makabila yote, mataifa yote na lugha zote kote duniani. Nawatakieni amani tele!

2. Nimeona vema kuwajulisha ishara na maajabu ambayo Mungu Mkuu amenionesha.

3. Jinsi gani zilivyo kubwa ishara zake Mungu!Maajabu yake ni makuu mno!Ufalme wake ni ufalme wa milele;enzi yake yadumu kizazi hata kizazi.

4. “Mimi, Nebukadneza, nilikuwa ninaishi raha mstarehe nyumbani kwangu na kufana katika ikulu yangu.

5. Lakini nikaota ndoto iliyonitisha; nikiwa nimelala kitandani, mawazo na maono kichwani mwangu yaliniogopesha.

6. Hivyo, nikaamuru wenye hekima wote wa Babuloni waletwe mbele yangu ili wanieleze maana ya ndoto hiyo.

7. Ndipo waganga, walozi, Wakaldayo na wanajimu wakaletwa. Nikawasimulia ndoto yangu, lakini hawakuweza kunieleza maana yake.

Kusoma sura kamili Danieli 4