Agano la Kale

Agano Jipya

Amosi 9:2-8 Biblia Habari Njema (BHN)

2. Wajapojichimbia njia ya kwenda kuzimu,huko nitawachukua kwa mkono wangu;wajapopanda mbinguni,nitawaporomosha chini.

3. Wajapojificha juu ya mlima Karmeli,huko nitawasaka na kuwachukua;wajapojificha mbali nami vilindini mwa bahari,humo nitaliamuru joka la baharini liwaume.

4. Wajapochukuliwa mateka na adui zao,huko nitatoa amri wauawe kwa upanga.Nitawachunga kwa makini sananiwatendee mabaya na si mema.”

5. Bwana Mwenyezi-Mungu wa majeshi,anaigusa ardhi nayo inatetemekana wakazi wake wanaomboleza;dunia nzima inapanda na kushukakama kujaa na kupwa kwa mto Nili wa Misri.

6. Mwenyezi-Mungu amejenga makao yake mbinguni,nayo dunia akaifunika kwa anga;huyaita maji ya bahari,na kuyamwaga juu ya nchi kavu.Mwenyezi-Mungu, ndilo jina lake!

7. Mwenyezi-Mungu asema hivi:“Kwangu mimi, nyinyi Waisraeli,hamna tofauti yoyote na watu wa Kushi!Niliwatoa Wafilisti kutoka Krete,na Waashuru kutoka Kiri,kama nilivyowatoa nyinyi kutoka Misri.

8. Mimi, Bwana Mwenyezi-Mungu nautazama ufalme wenye dhambi,na nitauangamiza kabisa kutoka duniani.Lakini sitawaangamiza wazawa wote wa Yakobo.

Kusoma sura kamili Amosi 9